Tathmini ya Mbinu za Mawasiliano katika Ufundishaji wa Lugha ya Kiswahili chini ya Elimu ya Mtaala wa Umilisi na Utendaji (CBC) katika Vyuo vya Ualimu, Kenya
Abstract
Utafiti huu ulitathmini ufanisi wa mbinu za mawasiliano katika ufundishaji wa Kiswahili chini ya Mtaala wa Umilisi na Utendaji (CBC), kwa kuangazia mazingira ya Chuo cha Ualimu cha Kitui kama mfano wa taasisi za mafunzo ya ualimu nchini Kenya. Kwa kutumia muundo wa mbinu mseto, data za kiasi zilikusanywa kutoka kwa wanafunzi wa ualimu (N = 120) na walimu wa Kiswahili (N = 12) kupitia dodoso la Likert. Data za ubora zilipatikana kupitia mahojiano ya kina na uchanganuzi wa nyaraka za ufundishaji wa Kiswahili. Matokeo yalionyesha matumizi ya kiwango cha kuridhisha ya mbinu shirikishi kama majadiliano ya kikundi, uigizaji, shughuli za mwingiliano, uandishi wa ubunifu, na mawasiliano ya kimatendo. Uchanganuzi wa takwimu ulionyesha uhusiano wa wastani wa nguvu kati ya kiwango cha matumizi ya mbinu shirikishi na utendaji wa wanafunzi (r = 0.47, p < 0.05). Changamoto kubwa zilijumuisha upungufu wa vifaa vya kufundishia, msongamano wa madarasa, muda mdogo wa vipindi, na ukosefu wa mafunzo endelevu kwa walimu. Utafiti unahitimisha kuwa mbinu za mawasiliano ni msingi wa kufanikisha CBC, lakini zinahitaji mazingira wezeshi, uwekezaji wa TEHAMA, na mafunzo endelevu ya walimu. Mapendekezo yanasisitiza hitaji la sera madhubuti, rasilimali stahiki, na tathmini ya kiutendaji inayolenga kujenga umahiri wa lugha miongoni mwa wanafunzi wa ualimu
Downloads
Published
How to Cite
Issue
Section
License
Copyright (c) 2025 Peter Karanja , Evelyne Kakivi Muthui

This work is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial 4.0 International License.
You are free to:
- Share — copy and redistribute the material in any medium or format
- Adapt — remix, transform, and build upon the material
Under the following terms:
- Attribution — Users must give appropriate credit, provide a link to the license, and indicate if changes were made. They may do so in any reasonable manner, but not in any way that suggests that you endorse them or their use.
- Non-Commercial — Users may not use the material for commercial purposes.
- No additional restrictions — Users may not apply legal terms or technological measures that legally restrict others from doing anything the license permits.